Thesuse na mama yake, Athera,
waliishi chini ya mlima mkubwa mahali palipoitwa Trozeni. Thesuse alipokuwa
angali mchanga baba yake, Egesu, aliinua jiwe kubwa lililokuwa mlimani katikati
ya msitu na hapo alilaza upanga na sapatu chini yake. kisha akamuambia Athera
kuwa Thesuse atakapokuwa mkubwa na mwenye nguvu za kuinua jiwe hilo basi
amfuate kule Atheni –huko Egesu alikuwa mfalme wa Attika.
Thesuse alipokuwa mkubwa, aliweza
kuchomoa ule upanga na sapatu kutoka chini ya jiwe na akafunga safari kuelekea
Atheni. Safari ya kuelekea Atheni haikuwa rahisi, ilikuwa na misitu mengi na
nyuma ya mawe makubwa walijificha majitu na majambazi. Lakini, Thesuse alimuaga
mama yake na kujaribu bahati yake. Hata hakuwa ameenda mbali sana alipovamiwa
na Perifite –aliyejulikana kwa utani kama “mbeba rungu.” Alionekana jamaa wa kutisha sana akiwa na
amebeba hiyo runga yake kubwa ya chuma. lakini Thesuse alimkabili na muda si
mrefu alikuwa amemwangamiza hapo barabarani. Akachukua hata hiyo rungu yakena
kuendelea na safari.
Mbele zaidi alikutana na Sinusi
“mkunja miti.” Ukatili wake ulikuwa wa kuwararua wasafiri kwa kuzinyambua miti
mbili kubwa na kisha kufunga msafiri kwa miti hizo na kuziwachilia zinepuke na
kumrarua mtega nyara huyo. Sinusi mwenyewe alikuwa pia na runga lakini haikuwa
na nguvu kama ile Thesuse alikuwa amebeba. basi siku hiyo ilikuwa Sinusi
aliyeraruliwa na miti hizo zenye mnaso. Akiendelea na safari alikutana na
jambazi aliyeitwa Sironi ambaye alilazimisha wasafiri wamwoshe mikuu hatimaye
aliwapiga teke na kuwaangusha kutoka ngomeni hadi baharini. lakini wakati huu
ilikuwa Sironi aliyepokea adhabu hiyo. Mbele kidogo paliishi jambazi mwingine
kwa jina Porokruste ambaye alijifanya kuwa mtu mkarimu na kuwakaribisha wageni
kwenye chumba chake lakini, wakipatikana kuwa warefu kuliko kitanda chake, aliwakata vichwa
au mikuu hadi watoshee. Na, wakiwa wafupi, aliwavuta shingo na miguu hadi
waliporefuka na kutoshea kitanda hicho. lakini pia Porokruste alipata adhabu
yake kama tu wale majambazi na majitu waliyomtangulia kwenye hii safari ya
kuelekea Atheni.
Wakati huo mrembo Medai ambaye pia
alikuwa mlozi mkubwa alikuwa akiishi kwenye ikulu ya mfalme. Alikuwa na mtoto
kijana aliyemtarajia kumridhi mfalme Egesu kwa hivyo alimtengenezea Thesuse
kinywaji kilichojaa sumu na kumwandalia kwenye kikombe kikubwa. Alimwambia
mfalme kwamba mgeni huyo wake alikuwa mkora ambaye alikuwa amekuja tu kumpokonya
ufalme wake na hivyo akamshawishi mfalme ampe Thesuse kinywaji hicho. Thesuse
hakujua njama hiyo na alikuwa ameshainua kikombe ili akunywe kinywaji wakati
Egesu alipoona ule upanga wake pamoja na sapatu na akakumbuka mwanawe. Aliruka
na kukichukua kikombe hicho chenye kinywaji hatari, na akakitupa mbali.
Medai alitumia mbinu zake na
akafaulu kujiponya na kutoroka. kwanza allita uchusichusi kutoka mtoni
ukamfunika. Kisha akaiita majitu yake yaliokuwa na mabawa na akaruka kwa gari
ambalo majitu hayo yaliivuruta na akatoroka Atheni- asirudi tena. Watu nao
hawakuchelewa kumweleza mfalme sifa zote za ujasiri wa Thesuse ambazo alizionyesha
katika safari yake kutoka Trozeni hadi kifika kwake Atheni. Egesu alifurahia sana
ngano hizo hata akatangaza siku tatu za kusherekea kuwasili kwa Thesuse. Lakini
kwenye hiyo harakati, alikuja mjumbe mmoja kutangaza kwamba wale wawia kutoka
Krete wamewasili.
Ilitokea kwamba hapo zamani, mwana
na mridhi wa mfalme Minoso wa Krete aliuawa na Waatheni. Na kulipiza kitendo
hicho, mfalme Minoso aliwashambulia Waatheni kwa kikosi chake kikubwa cha jeshi
na kuwalazimu Waatheni kukubali masharti yake ambayo yalikuwa kwamba kila baada
ya miaka tisa watampa ‘watoto wa kafara’ ambao walikuwa wanaume saba na mabinti
saba. Naye aliwachukua hao ‘watoto wa kafara’ na kuwatupa kwa jitu moja kubwa
liloitwa Minota ambalo ingawa kiwiliwili chake kilikuwa cha mtu, kichwa chake
kilikuwa cha fahali. Minota aliishi pangoni huko Krete Karibu na ikulu ya
mfalme. Pango hilo lake lilikuwa na njia nyingi ambazo zilimchanganya yeyote
aliengia humo. Hakuna hata mtu mmoja aliyefaulu kurejea kutoka humo pangoni mara
tu alipoingia.
Thesuse aliamua kwamba ataangamiza
jitu hilo na kukomesha dhuluma hiyo duni ya kuwaua watu kumi na wane wasio na
hatia kila baada ya miaka tisa. Na basi, hata kabla ya kuchaguliwa wale vijana
ambao wangepelekwa Krete, Thesuse alijitolea muhanga na wale wengine
wakachaguliwa kwa kupigiwa kura kama ilivyokuwa desturi. Jambo hilo la Thesuse
kujitolea kivyake lilimletea umaarufu sana mbele za watu. Muda si muda,
merikebu iliyowabeba watoto hao wa kafara ilinoa nang’a huku imevikwa tanga ya
rangi nyeusi kama ilvyokuwa kawaida ila wakati huu mfalme Egesu alimpa mwanawe
tanga ingine nyeupe ili aipeperushe kwa merikebu kama atakuwa bado hai wakati
wa kurejea.
Walipowasili Krete Thesuse
hakuchelewa kumweleza mfalme Minoso kwamba nia yake ilikuwa Kumuua jitu Minota.
Minoso alikubali ombi la Thesuse kwamba akifaulu basi yeye na wale wanakafara
wengine wataachiliwa huru na tena deni lake litakuwa limelipwa milele. Hata
hivyo, Minoso aliongeza sharti kwamba Thesuse ataingia mle pangoni bila upanga
wake kuenda kukabiliana na jitu.
Hapo kwa dari ya chumba ambacho
walikuwa wamefungiwa Thesuse na wenzake palikuwa chumba cha binti zake mfalme
Minoso, Ariadin na Faidera ambao waliamua kumsaidia Thesuse katika juhudi zake.
Walifungulia Thesuse mlango kama wale wengine bado wamelala na kumpeleka hadi
palipokuwa hiyo pango maarufu lenye kuta za marumaru zilizong’a kwenye mwangaza
wa mwezi. Ariadin alimfichulia “Wakati huu ndiyo mzuri wa kuua jitu hilo kama
lingali linalala. Usiongojee hadi asubuhi likishaamka” Ariadin aling’ong’oza. “Maskani
yake ni humu katikati mwa pango hili lenye njia nyingi zenye mikato aina ya
labiranthi. Fuata sauti ya mg’oroto wake. Pia chukua upanga huu na kipira cha
uzi ambao utatumia kupata njia ya kurejelea kutoka pangoni” Kwa hayo maneno,
ariadin alibaki kama ameushika mwanzo wa uzi na Thesuse akaingia na mradi
wenyewe akiachilia polepole kwa kuelekea ndani, upanga nao thabiti mkononi.
Mle ndani njia zilikuwa kabibu na
nyingi zilikuwa na wa mkingo wa gafla bila kuelekea popote na hapo Thesuse
ilimbidi arudi nyuma na kutafuta tena. Inasemekana kuwa hapajawai kuwa na
mikato za labirathi zilizokuwa za kutatiza kama hizi zilizotengenezwa na
mhandisi Dadesulu. Ingia ndani, toka tena; ingia Thesuse aliendelea. Alizidi
kusikia sauti ya kung’orota kwa Minota ikiongezeka na kujua kwamba anakaribia
makao yake. Kwa hayo yote Ariadin na Faidera waliongojea langoni, Ariadin
akishikilia upande wake wa uzi kwa ustadi. Mara walisikia mtetemeko mkubwa na
yowe kwa mbali kisha kukawa na kimya kikuu. Ariadin hangeweza kujua kama
Thesuse ameuawa au kama hata bado alikuwa na ule mradi ulioviringishwa uzi
lakini alianza kuhisi uzi ukivutuavutua halafu muda si mrefu mwana wa mfalme
Egesu akajitokeza.
Ile meli iliyowaleta Thesuse na
wenzake Krete ilikuwa bado pale ufuoni. Vijana walikuwa wangali wanalala
walipoamshwa na mara moja walikuwa safarini kurudi Atheni. Nao pia Ariadin na
Faidera kwa kuhofia hasira ya baba yao, waliwafuata. Katika safari hiyo walitua
kwenye kisima cha Nakso na wakatengeneza kambi hapo kwa miamba usiku. Kesho
yake asubuhi na mapema waliendelea na safari hiyo yao lakini Ariadin alibakia
kama amelala na kwa hivyo aliwachwa nyuma. Thesuse hakusahau tu Ariadin ila pia
kupeperusha ile tanga nyeupe baba yake alikuwa amempa. Kwa hivyo meli yao
ilipojitokeza Atheni na tanga nyeusi juu yake mfalme Egesu alijitupa baharani
akidhani kuwa mwanawe hakufaulu.
* Ariadin alichukuliwa na Bachisu
akampeleka angani na kumvisha taji iliyo na nyota tisa kichwani. Yeye huonekana
hadi leo angani ya kaskazini.