Friday 24 April 2015

LORENZO

Lorenzo: Che meingia, usiku achekelewa

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Kwa miale yake mawingu azikata

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Na kutawanya giza aliyezagaa

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Kama mayungi majini yanavyolewa

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Jua laoneka wazi. Litazunguka

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Falaki yake likiangaza mimea.

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Lilo jicho lake Mungu huchemsha anga

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Hapa bustani lazima nipande tuka


&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Mama ardhi ni mwenye miujiza kweli.

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Mji mwake ndimo tukifa huzikwa sisi

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Na huzalishwa dhuria mwake tumboni

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Ambao huwa mlo aina anuwai

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Kwa viumbe vyote vilio na uhai.

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Alamina kujaza dunia arzaki

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Majaza yasiyokuwa nacho kifani

&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp&nbsp Alhasili: miti, mawe nazo madini


&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Yote chimbuko yao ni ardhini hapa

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Walakini shida huwa yeye ingawa

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Huzingatia kuleta yaliyo mema.

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Wengine nao huyatumia vibaya.

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Ila, isipokuwa kwa nahusi. Badala

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Insafu nuiwa. Patukia ukuba

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Usio wa kutazamiwa. Mfano mmoja

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Ni hili ua: Ni sumu tena ni dawa.


&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Ukililamba unakufa wako mwili

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Kilinusa, unachechemka wote mwili.

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Zimefanywa zote hizo mardufu kazi

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Kwa kutumiwa kitu kimoja tu hiki.

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Hivyo hata binadamu tulivyo nafsi

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Tuna hisani pamoja na uhasidi

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Maulana basi ubaya yetu ndani

&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160&#160 Sije tawala juu yake hasanati.

Wednesday 7 January 2015

TANZU TATU ZA FASIHI


Hakika hamna tanzu ya fasihi iliyo bora kuliko nyingine. Kama vile jazanda ya mti ilivyoonyesha. Tanzu zote tatu zinatoshana barabara kwa hadhi ya kuakilisha fasihi. Iwe

(i) Andishi (matawi): inayokumbatia riwaya, tamthilia na diwani;

(ii) Simulizi (majani): inayokumbatia tamba, kukariri, kuimba na mijadala; au

(iii) Onyeshi (maua): inayokumbatia uigizaji, tamasha kama vile denzi na mieleka na sinema.

Tunapotaka kutathmini ubora wa fasihi vipo vigezo vinavyotumika ambavyo hutangulia na kutofautisha fasihi katika sehemu mbili maarufu: (a) fasihi dhati na (b) fasihi pendwa